- 2,513 viewsDuration: 2:38Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetangula amezitaka kamati za bunge kutowadhalilisha wanaofika kutoa taarifa kuhusu maswala yanayoibuliwa. Akizungumza kwenye ufunguzi rasmi wa kongamano la wabunge, Wetangula ameeleza kuwa afisi yake imepokea malalamishi kutoka kwa baadhi ya watu wanaodai kufedheheshwa kwenye vikao vya kamati za bunge. Wetangula ametoa mfano wa inspekta jenerali wa polisi, na maafisa wa tume ya walimu ambao. Aidha wetangula amewataka wabunge kuwajibika akiwaonya kuwa utepetevu utawakosesha nafasi ya kuchaguliwa tena kuwawakilisha wananchi.