- 239 viewsDuration: 1:48Wakazi katika Wadi ya Cheragita katika eneo bunge la Ol-Joro Orok wanalalamikia kukithiri kwa visa vya wizi wa mifugo na mali nyingine. Wanadai vijiji vya Olaimuta, Ruiru na Gichure ndivyo vilivyoathiriwa zaidi na visa hivyo huku wakaazi wa eneo hilo wakiomba hatua za dharura kuchukuliwa . Wakazi hao wamesema wamekuwa wakikesha usiku kucha ili kulinda mifugo wao wasiibwe.