- 1,874 viewsDuration: 5:04Wananchi, wahudumu wa sekta ya uchukuzi na viongozi mbalimbali wanaitaka serikali kuweka mikakati zaidi ya kupunguza gharama ya mafuta wakisema hatua iliyoafikiwa jana ya kupunguza ushuru wa vat hautoshi. Wakenya wanasema kuwa ongezeko la petroli kwa zaidi ya shilingi 19 na dizeli kwa zaidi ya shilingi thelathini unaowaongezea mzigo mkubwa wa gharama ya maisha huku wakihofia kugharamika zaidi wanafunzi watakapofungua shule katika wiki mbili zijazo.