- 1,598 viewsDuration: 3:31Waziri wa Kawi Opiyo Wandayi anashikilia kuwa hakujua lolote kuhusu sakata ya uagizaji wa mafuta nje ya mpango wa serikali, akisema kamati maalum ya kukagua viwango vya mafuta nchini iliidhinisha uagizaji huo. Wandayi amesisitiza kwamba hatajiuzulu kutokana na sakata hiyo, akisema uchunguzi unaoendelea utamwondolea makosa. Kumekuwa na tumbojoto nchini ya kutaka Wandayi ajiuzulu huku bei ya mafuta ikitarajiwa kubadilishwa hapo kesho.