Zaidi ya watu 8,000 wamefaidika na kambi ya matibabu iliyoandaliwa katika eneo la Thika, kaunti ya Kiambu.
Kambi hiyo ya matibabu iliyoandaliwa kwa siku tatu na shirika la Shree Jain Youth League, ilitoa matibabu ya macho, masikio na koo kwa
zaidi ya wakazi mia nne. wataalamu kutoka india walishirikiana na madaktari wa humu nchini. Wagonjwa wengi wa macho wameathirika na ugonjwa wa mtoto wa jicho na shinikizo lndani ya jicho au glakoma. Madaktari wanasisitiza haja ya kupunguza gharama ya matibabu ili wakenya wengi wapate matibabu maalum.