Kenya na Japan zimejitolea kuimarisha ushirikiano wa kibiashara, uwekezaji, maendeleo na mashauriano katika sekta mbalimbali. Waziri mwenye mamlaka makuu aliye pia waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Musalia Mudavadi alikuwa mwenyeji wa ujumbe wa serikali ya Japan ukiongozwa na waziri wa mambo ya nje wa Japan, Motegi Toshimitsu, ambako alisema taifa hili linatambua umuhimu mkubwa wa ushirikiano wake na Japan, ambao unaendelea kuwasilisha matokeo halisi katika sekta muhimu za uchumi.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive