Baadhi ya viongozi wa Magharibi ya nchi waendelea kupinga ukodeshaji wa viwanda

  • | Citizen TV
    1,648 views

    Baadhi ya viongozi wa Magharibi ya Nchi wamemrai Rais William Ruto kusitisha mkataba wa kukodisha viwanda vya sukari kwa mwekezaji wa kibinafsi, Jaswant Rai . kulingana nao, uamuzi wa kukodisha viwanda hivyo ni dhihirisho kwamba serikali ya Kenya Kwanza imefeli kuzingatia manifesto yake hasa kipengele cha kufufua uchumi wa eneo la magharibi.