Siasa za urithi wa mwaka 2032 ziliibuka katika eneobunge la Maara kaunti ya Tharaka Nithi wakati wa hafla ya uwezeshaji jamii kiuchumi. Viongozi wa Kenya kwanza walimhimiza naibu rais Kithure Kindiki kuwania kiti cha urais pindi muhula wa Rais Ruto utakapokamilika. Kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa Kimani Ichung’wa katika kumuunga mkono, alisema Kindiki ndiye mwaniaji anayefaa kuwania wadhifa huo. Kindiki ambaye alikuwa akiongoza mpango huo wa uwezeshaji wakazi kiuchumi, alikwepa suala hilo na badala yake akakosoa mrengo wa upinzani kwa kile alichosema ni kueneza siasa za migawanyiko. Abdiaziz Hashim ana taarifa kwa kina.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive