- 316 viewsDuration: 3:22Utafiti wa shirika la kitaifa kuhusu takwimu za watu - KDHS -wa mwaka wa 2022 unaashiria kuwa ni idadi ndogo sana ya kina mama kutoka jamii zinazoishi kaskazini mwa nchi wanaojitokeza kupata vipimo vya saratani. Hali hiyo imesababisha kampeni ya kutoa hamasa kwa kina mama katika maeneo hayo kufanywa kwa njia tofauti sana. Wataalamu wa saratani wanafanya vikao vya usiku katika manthari ya kitamaduni ili kuwafahamisha na kuwashirikisha kina mama katika juhudi za kukomesha ugonjwa wa saratani ya mlango wa uzazi. Bonface Barasa anaarifu zaidi.