- 31 viewsDuration: 2:38Vijana katika kaunti ya Kilifi wamehimizwa kujiunga na taasisi za kiufundi ili kupata ujuzi utakaowawezesha kunufaika na ajira zinazotokana na sekta ya uchumi wa baharini. Wadau waliozungumza katika uzinduzi wa masomo ya upishi katika taasisi ya Muyeye Vocational Training Centre, Malindi, walisema mafunzo hayo yatawajengea vijana uwezo wa kushindana katika soko la ajira la humu nchini na kimataifa.