- 39 viewsDuration: 1:26Viongozi wa kijamii pamoja na baadhi ya wakaazi wa kaunti ya Mombasa wamekemea ongezeko la visa vya mauaji ya wanawake nchini na kuitaka serikali kuwachukulia hatua kali wahusika wa vitendo hivyo. Wakiongozwa na Mkurugenzi wa Alfayo Foundation, Nelson Alfayo, viongozi hao walisisitiza umuhimu wa kudumisha amani, uvumilivu wa kisiasa na kuwawezesha wanawake pamoja na vijana katika jamii.