- 321 viewsDuration: 2:05Wakaazi wa Diani wanaodai kuwa walikua wamiliki wa mashamba ya kipande cha ardhi cha Block 10 wametaka agizo la mahakama la mwaka wa 2019 la kufutilia mbali hati miliki 560 zilizosemakana kupatikana kinyume cha sheria kutekelezewa ili wenyeji waregeshewe mashamba yao. Wakaazi hao wanasema serikali imekua ikijikokota kutekeleza agizo hilo huku ardhi hizo zikiendelea kuingiliwa na mabwanyenye wakitumia hati hizo zilizoharamishwa na mahakama. Wameibua wasisi kua baadhi ya maafisa wa polisi wamekua wakitumika kusimamia ujenzi wa kuta na mijengo kadhaa eneo hilo.