- 264 viewsDuration: 1:19Muungano wa vyama vya wafanyakazi nchini COTU umesuta shirikisho la waajiri nchini FKE kwa kile unachodai ni kutoa taarifa za kupotosha kuhusu nyongeza ya asilimia 12 ya mishahara. Sasa katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli ameitaka serikali kumchukulia hatua Mkurugenzi wa FKE Jackline Mugo akisema hatua hiyo inakinzana na mwongozo wa serikali. Rais William Ruto alitangaza Nyongeza hiyo wakati wa maadhimisho ya sikukuu ya leba dei.