- 485 viewsDuration: 4:31Idadi kubwa ya wanawake katika Kaunti ya Samburu wameathirika na mila zinazolemaza ndoto zao, hasa ndoa za mapema zinazowanyima fursa ya elimu. Hata hivyo, Christine Leseewa, ambaye ni mama wa watoto sita na anayehudumu kama kasisi, ni mfano hai wa waathiriwa hao lakini hakukata tamaa. Katika makala ya mwanamke bomba wiki hii, Leseewa anasimulia jinsi alivyokabili changamoto hizo na kuasisi duka la kwanza la kuuza vitabu Samburu.