Skip to main content
Skip to main content

Utafiti wa TIFA waonyesha imani ya Wakenya kwa Ruto yakwama chini

  • | Citizen TV
    629 views
    Imani ya Wakenya kwa Rais William Ruto inazidi kushuka huku utafiti wa shirika la TIFA ukionyesha kuwa asilimia 68 ya Wakenya hawana imani naye. Kwa mujibu wa utafiti huo, Wakenya pia wamekosa imani na taasisi muhimu za serikali, zikiwemo idara ya polisi, bunge na IEBC. Zaidi ya theluthi mbili ya Wakenya wanaamini nchi inaelekea pabaya huku gharama ya maisha ikizidi kupanda na hali ya uchumi ikiendelea kuwa ngumu.